Utangulizi
Parokia ya Mt. Thomas More (Mbezi Beach) iko katika Jimbo Kuu la Dar es Salaam chini ya Dekania ya Mt. Thomas More katika Manispaa ya Wilaya ya Kinondoni, Mkoa wa Dar es Salaam. Parokia hii inapakana na Parokia Jirani za Bikira Maria Mama wa Huruma, Mtakatifu Gasper De Bufalo na Mtakatifu Mikael Malaika Mkuu, Kawe.
Parokia ya Mt. Thomas More ina historia ndefu ambapo mwaka 1996 baada ya kibali cha Paroko wa Parokia ya Tegeta, waamini walianza kusali kwenye kikanisa kidogo cha Masista wa Shirika la Waabuduo Damu Azizi ya Yesu, Mbezi Beach, kilichokuwepo pale lilipo kwa sasa Kanisa la Bikira Maria Mama wa Huruma, Mbezi Beach. Baada ya Kanisa la Bikira Maria Mama wa Huruma kutangazwa kuwa Parokia mpya, bado hiyo Parokia ilionekana kuwa mbali na makazi ya waamini wengi wa Mbezi Beach na hivyo mpango ukafanyika kufanyia ibada kwenye ukanda wa pwani karibu na Bahari na hatimaye ukapatikana ukumbi kwenye makazi ya Benki Kuu ya Tanzania yaliyopo eneo hilo ambapo ibada za Jumapili ziliadhimishwa hapo.
Paroko's statement to be entered here
Father Adrian Mubezi
Mwaka 2005 Jumuiya Ndogo Ndogo za Kikristu tatu (03) zilikuwa zinasali pamoja katika ukumbi wa makazi ya majengo ya BOT Mbezi Beach nazo ni;
- Mt. Thomas More
- Mt. John Fisher
- Familia Takatifu
Uanzishwaji wa kigango cha Mt. More
Jumuiya hizo tatu zilizotajwa hapo juu zilishirikiana na kuratibu uanzishwaji wa Kigango kwa kushirikiana na Uongozi wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Huruma Mbezi Beach, Dar-es-salaam.
Kigango kuitwa jina la Mt. Thomas More lilihasisiwa na moja ya Jumuiya tatu anzilishi zilizotajwa hapo juu. Baadhi ya wanajumuiya katika jumuiya hiyo walikuwa wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Mt. Thomas More ambayo baada ya kuchukuliwa na serikali ikaitwa Shule ya Sekondari ya Ihungo iliyoko Mkoa wa Kagera. Wanajumuiya wa Jumuiya zote tatu zilizotajwa hapo juu kwa pamoja walikubaliana Kigango kiitwe Mt. Thomas More na kuwakilisha mapendekezo yao kwa Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.
Mwezi Agosti 2005, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo aliridhia mapendekezo yao na kuundwa kwa Kigango kipya kilichojulikana kama Kigango cha Mt. Thomas More na hatimaye hata Parokia kutumia jina la Mtakatifu huyo. Historia ya maisha na kifo chake Mt. Thomas More inapatikana katika vitabu mbalimbali, majarida mbalimbali na mitandao ya Kanisa Katoliki. Kumbukumbu yake ni tarehe 22 Juni kila mwaka.
Baada ya kuundwa kwa Kigango cha Mt. Thomas More, Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Huruma Padri Romuald Mukandara alisitisha kutumia Ukumbi wa BOT kwa huduma za Kiroho na kushauri kutafuta eneo litakalojengwa Kanisa kwa ajili ya huduma hiyo.
Waamini wa Jumuiya hizo walianza mkakati wa kutafuta Kiwanja cha kujenga Kanisa na kufanikiwa kupata Viwanja namba 139,140 na 141 Kitalu namba. 34 vilivyoko Mbezi Beach A, Dar-es-Salaam. Ujenzi wa Kanisa dogo ulianza tarehe 19/09/2005 kwa michango ya Waamini na kumalizika tarehe 24/09/2005 kazi iliyofanyika ndani ya muda wa wiki moja na Waamini walihama kutoka Ukumbi wa BOT na kuanza kusali katika Kanisa hilo dogo tarehe 25/09/2005.
Misa ya uzinduzi wa kigango
Kigango cha Mt. Thomas More kikiwa chini ya Parokia ya Bikira Maria Mama wa Huruma kilizinduliwa rasmi tarehe 18/10/2005 katika Misa ya uzinduzi iliyoongozwa na Padri Stephano Kaombe. Wakati huo Kigango kilikuwa na jumla ya Waamini 785.
Wakati wa uzinduzi kulifanyika:
- Harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa jipya
- Kuunda uongozi wa Kigango kwa kuchagua Kamati Tendaji
- Kuunda Kamati ya maendeleo ya Kigango ambayo iliundwa kutokana na viongozi wa Kigango na Kamati Tendaji za Jumuiya.
- Kushughulikia ujenzi wa kanisa la muda kwa kufanya uboreshaji na upatikanaji wa vifaa kwa ajili ya Misa na vitu muhimu kama viti vya kutumia Kanisani.
- Ujenzi wa choo cha muda kwa matumizi ya Waamini wakati wa Misa, na kuvunja jengo bovu lilokuwa karibu na Kanisa la muda na ambalo lilikuwa ni hatari kwa Waamini hasa watoto.
Uchaguzi wa viongozi wa kwanza
Uchaguzi wa viongozi wa Kigango ulifanyika tarehe 20/11/2005 chini ya usimamizi wa Bwana Sangu kutoka Jimboni na viongozi wafuatao walichaguliwa:
- Marehemu Frank Makwai - Mwenyekiti wa Kigango
- Bw. Moses Nombo - Makamu Mwenyekiti wa Kigango
- Bw. Joseph Selesi - Katibu wa Kigango
- Bw. Edward Sungula –Katibu Msaidizi wa Kigango
- Bw. Kened Nyoni - Mweka Hazina wa Kigango
Jiwe la msingi
Tarehe 07/01/2006, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo alikuwa mgeni rasmi, alibariki na kuweka Jiwe la Msingi katika kiwanja ambacho Kanisa la kudumu litajengwa. Tukio hilo lilishuhudiwa pia na Hayati Mh. Edward Lowasa (aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania wakati huo) kama mgeni wa rasmi.
Kigango cha Mt. Thomas More chahamishwa kutoka parokia ya bikira maria mama wa huruma
Kigango cha Mt. Thomas More kilihamishwa kutoka Parokia ya Bikira Maria Mama wa Huruma na kuwa chini ya usimamizi wa Parokia ya Mt. Gaspari del Buffalo kuanzia mwaka 2010 mpaka mwaka 2014.
Ukuaji wa kigango
Baada ya muda Jumuiya ya Moyo Mtakatifu wa Yesu ilianzizishwa. Jumuiya hii pamoja na Jumuiya za Thomas More na Familia Takatifu zikagawanywa na kuzaa Jumuiya za Damu Takatifu ya Yesu, Theresia wa Mtoto Yesu na Kristu Mfalme hivyo kufanya Kigango kuwa na jumla ya Jumuiya Saba (07) kama ifuatavyo:
- Mt. Thomas More
- Mt. John Fischer
- Familia Takatifu
- Moyo Mtakatifu wa Yesu
- Theresia wa Mtoto Yesu
- Damu Takatifu ya Yesu
- Kristu Mfalme
Kuteuliwa kigango cha Mt. Thomas More kuwa Parokia
Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo alikiteua Kigango cha Mt. Thomas More kuwa Parokia Teule tarehe 07 Julai 2014 na kuwa Parokia kamili tarehe 07 Julai 2015 na Paroko wa kwanza alikuwa Padri Gilbart Makuru tangu ilipokuwa Parokia Teule 2014 mpaka Julai 2015.
Maporoko wengine walioteuliwa kuongoza Parokia ya Mt. Thomas More ni kama ifuatavyo:
| Jina | Muda |
|---|---|
| Paroko Nicolaus Masamba | Julai 2017 – Julai 2018 |
| Paroko Audax Kaasa | Julai 2018 – Julai 2022 |
| Paroko Ladislaus Kapinda | Julai 2022 – Septemba 2024 |
| Paroko Sylivanus Bwito | Septemba 2024 – Machi 2025 |
| Paroko Aidan Mubezi | Machi 2025 – Hadi sasa |
Ujenzi wa kanisa jipya
Kama ilivyoelezwa hapo juu Kanisa lililojegwa hapo awali lilikuwa ni la muda. Ujenzi wa Kanisa jipya ulianza rasmi mwaka 2011. Waumini walihamasishana kuchangia ujenzi wa Kanisa jipya na muitikio ulikuwa mkubwa. Ingawa kulikuwa na changamoto nyingi zilizojitokeza hasa ukizingatia kuwa eneo lenyewe lilikuwa na bonde na udongo wa mfinyanzi, ikapelekea ramani yake ifuate umbile bonde hilo ili kuhakikisha kuwa kiwanja hicho kinatumika ipasavyo.
Ramani ya jengo hilo imegawanyika katika sehemu kuu tatu (3), sehemu ya kwanza ni chini kabisa ambapo tunasali sasa na kimpangilio pale ni ukumbi. Sehemu ya pili juu katikati ni ukumbi, ofisi ya Paroko, Paroko Msaidizi na vyama vya Kitume. Sehemu ya tatu (3) ndilo kanisa lenyewe
Ukuaji wa parokia
Parokia kwa sasa ina idadi ya waamini walio hai takriban elfu mbili (2,000) na jumla ya jumuiya ishirini na tisa (29) ambazo zimeunda kanda nane (8). Nazo ni:
| Jina la Kanda | Jina la Jumuiya Zinazounda Kanda |
|---|---|
| Bethlehem | Mt. Mikael Malaika Mkuu |
| Mt. Monica | |
| Mt. Rita wa Accasia | |
| Mwenye Heri Isdori Bakanja | |
| Bethania | Mt. Andrea Mtume |
| Familia Takatifu | |
| Mt. Benedicto Abate | |
| Mt. Fransisco wa Asizi | |
| Galilaya | Kristu Mfalme |
| Moyo Safi wa Maria | |
| Mt. Maria Margaret Alakoque | |
| Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili | |
| Nazarethi | Mt. Dominico |
| Mt. Martha | |
| Mt. Joseph | |
| Kaanani | Mt. Padre Pio |
| Damu Takatifu ya Yesu | |
| Yerusalemu | Mt. Thomas More |
| Mt. Maria Magdalena | |
| Samaria | Mt. Augustino |
| Mt. John Fischer | |
| Mt. Maria Faustina | |
| Theresia wa Mtoto Yesu | |
| Mt. Vicent De Paul | |
| Yeriko | Mt. Petro |
| Mt. Yohana Mbatizaji | |
| Mt. Paulo Mtume | |
| Mt. Elizabeth wa Hungaria |
Utoaji wa sakramenti mbali mbali
Tangu kanisa la Mt. Thomas More kuanzishwa kama Parokia rasmi mwaka 2015 mpaka sasa idadi ya waamini waliopata sakramenti mbali mbali zilizotolewa ni kama ifuatavyo:
- Wakristo wapya (watoto na watu wazima kutoka ukatekumeni) waliobatizwa ni - 839
- Waamini waliopata Kipaimara ni - 463
- Waamini waliofunga ndoa ni -132
Wote hao ni kutoka katika jumuiya zilizotajwa hapo juu. Mwezi Julai 2024 Parokia hii ya Mt. Thomas More ilibarikiwa kutoa Padre anayetoka kwenye familia moja ya waamini wa Parokia, ambaye jina lake ni Padre Manfred Semda. Padre Semda kwa sasa anahudumu katika Seminari ya Visiga. Hakika ni jambo la kumshukuru Mungu kwa aliyotutendea kwa kutuwezesha kupata Padre mzawa wa Parokia yetu. Tunamwomba Mungu aendelee kuwagusa na watoto wetu wengine ili wapate wito wa kuwa watawa.
Maendeleo ya ujenzi wa kanisa
Mradi wa ujenzi wa kanisa bado unaendelea na sehemu kubwa ya Kanisa imeishajengwa, kilichobaki ni umaliziaji wa jengo katika sehemu mbalimbali kama ifuatavyo:
- Maboresho ya minara yetu ili tukamilishe uwezekaji wa paa lote
- Matengenezo ya njia ya wahitaji (disabled)
-
Maboresho mengine yanayotajwa kumaliziwa ili tuanze finishing ni:
- Maboresho ya mlango mkuu wa kuingia
- Vyumba vya maungamo na ngazi za kufika kwa urahisi katika minara yetu
- Baada ya hapo ni hatua za umaliziaji wa kanisa letu kadri ya uongozi wa wataalamu na wasimamizi wetu wa mradi huu.
Hitimisho
Tunamshukuru sana Mungu kwa kutuwezesha sisi waamini wa Parokia ya Mt. Thomas More kufikia maendeleo tuliyonayo kwa kipindi cha miaka kumi tangu Parokia yetu ianzishwe, hasa ya kulijenga kanisa la Mungu na pia kuwawezesha waamini kupata huduma za kiroho na kupata sakramenti mbalimbali. Tunamwomba Mungu aendelee kutupa nguvu na afya njema ili tuweze kulikamilisha kanisa letu jipya.
Tumapenda pia kuwashukuru waamini wote wa Parokia kwa kujitolea kwa hali na mali katika ujenzi wa kanisa letu, pia kwa kushirki kikamilifu katika shughuli za kiroho. Tunawashuru Maparoko wote waliohudumia Parokia yetu bila kuchoka kwa kipindi hiki cha miaka kumi. Mungu awabariki sana.
Shukrani za kipekee ziwaaendee hawa wafuatao:
- Mhashamu Askofu Mkuu wa jimbo kuu la Dar es salaam Baba Thadeus Ruwaichi pamoja na viongozi wa Jimbo kwa kuwa nasi na kutusaidia kwa njia mbalimbali za kiroho pia kuliendeleza na kulijenga kanisa letu. Ahsante sana Baba yetu
- Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo – Aliyekuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam ambaye alikuwa nasi na bado tuko naye, kutoka kipindi cha uanzishaji wa Kigango mpaka kuweka jiwe la msingi wa kulijenga kanisa letu. Mungu ambariki sana